Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa rumande kwa siku 21 mwanamke mmoja anayekabiliwa na shtaka la kumuuwa mwanawe kwa kumzika akiwa hai.
Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa ametoa agizo hilo baada ya upande wa mashtaka kuiomba Mahakama kumpa muda zaidi ili kuwawezesha maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo kukamilisha uchunguzi wao.
Kulingana na upande wa mashtaka ukiongozwa na Nancy Njeru ulieleza Mahakama kwamba mtoto huyo alikuwa ameishi siku mbili baada ya kuzuiliwa.
Mahakama imeelezwa zaidi kwamba kabla ya mshukiwa kumzika mtoto huyo akiwa hai, ni lazima mwanamke huyo alikuwa na tatizo ndiposa upande wa mashtaka uanitaji muda zaidi kwa kufanya uchunguzi sawa na kumhoji mshukiwa.
Mshukiwa Maua Karisa anadaiwa kumzaa mwanawe tarehe 24 Mei 2026, na kutekeleza kitendo hicho tarehe 26 Mei 2026 katika eneo la Matsangoni kaunti ya Kilifi.
Kesi hiyo itatajwa tarehe 22 mwezi Juni mwaka huu.
Taarifa ya Tecla Yeri
